Macho na masikio ya Watanzania wengi kwa siku ya Jumamosi June 07 yote yalielekezwa Durban Afrika Kusini sehemu ambako zilikua zikitolewa tuzo za wateule wa MTV Afrika Music Award ‘MAMA’.
Furaha na matumaini ya Tanzania yalikuwa kwa kijana wa nyumbani, Diamond Platnumz ambaye ameingia katika tuzo hizo kwa mara ya kwanza.. Diamond aliteuliwa kuwania tuzo hizo katika vipengele viwili, Best Male artist, na Best collaboration Song. Bahati haikuwa njema sana kwani Diamond hakufanikiwa kupata tuzo hizo..
Diamond Platnumz alikuwa pia ni moja kati ya watumbuizaji wa ugawaji wa tuzo hizi,ambapo kwa namna alivyoingia kwenye jukwaa na Davido ilimfurahisha kila mtu aliyekuepo ukumbini na watu waliokuwa wakiangalia nyumbani kupitia Television.