Blogger Widgets

Saturday, June 15, 2013

BREAKING NEWS!!! BOMU LAKUTEGWA LALIPUKA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA WAKATI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI WA MADIWANI ARUSHA.



Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba, kumetokea mlipuko wa bomu linalosadikiwa ni la kutegwa, katika mkutano wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kampeni za udiwani Arusha, maeneo ya viwanja vya Soweto, kaloleni Arusha. Mpaka sasa habari zilizotufikia ni kwamba watu wawili wamepoteza maisha, na majeruhi wanakimbizwa hospitali ya mkoa MT.Meru.
Mkutano huo ndio ulikuwa wa mwisho kabla ya uchaguzi wa madiwani hapo kesho. Mh. Freeman Mbowe nae alikuwa moja ya watu waliohudhuria mkutano huo. Habari zaidi zitakujia kutoka hapa!