Blogger Widgets

Wednesday, February 10, 2016

New Music: Listen, Download and Support this Upcoming Artist..



Kwa support tuliyopata toka kwa Viewers wa blogyetu toka kuanzishwa kwake ndiyo iliyotufikisha hapatulipo,, And now its our turn to pay back. This is us supporting Underground Music, trying to take Tanzanian Music to that New Level,, KWa Moyo Wa Dhati tunakuomba Sikiliza na Download Nyimbo hii toka kwa Msanii Mchanga Bless, Then Tupe maoni yako kusaidia kuendeleza mziki wa kizazi kipya Tanzania.

Tumerudi Tena na Hizi za Mkude Simba, Sikiliza na Download Hapa..

Baada ya kimya Kirefu, Sasa tunarudi tena na hizi kutoka Kwa Mkude Simba,, Bofya hapa Kusikiliza na ku Download...

Wednesday, October 28, 2015

HAYA NDIO MAAMUZI MAPYA JUU YA UCHAGUZI WA ZANZIBAR..!!



MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR YAMEFUTWA, Madai ni kuwa uchaguzi huo haukuwa wa huru na Haki
Sababu nyingine iliyochangia kufutwa kwa matokeo hayo ni pamoja na ikiukwaji wa sheria ikiwemo mgombea Maalim Seif kujitangaza kwenye matokeo kuwa mshindi.
Via AzamTV

Thursday, September 3, 2015

SIRI, HOTUBA YA DK. SLAA..

Hotuba ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, imepondwa vikali na wasomi mbalimbali wasiofungamana na upande wowote kisiasa.
Juzi Dk. Slaa baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kufuatia kujiweka kando kujishughulisha na Chadema kutokana na na chama hicho kumpokea Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa na kumpitisha kugombea nafasi ya urais akiviwakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ajitokeza hadharani na kutoa msimamo wake wa kustaafu siasa, huku akimtuhumu mgombea huyo kuwa alihusika moja kwa moja na sakata la Richmond, jambo ambalo limezua mjadala mkubwa kwa jamii.
Mkufunzi Msaidizi kutoka Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma (SJMC) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Godlisten Malisa, alipotakiwa na Nipashe kutoa maoni yake, alisema pamoja na kukubaliana na hotuba ya Dk. Slaa, lakini haikutolewa katika muda muafaka.
“Dk. Slaa ni kiongozi anayeheshimika kutokana na mchango wake mkubwa wa kuuimarisha upinzani na hasa Chadema, lakini alichokisema na hasa dhidi ya Lowassa kilipaswa kusemwa wakati wa mchakato wa kumpokea Chadema ama kabla ya kuingia kwenye kipindi cha kampeni,” alisema.
Malisa alisema, alipaswa kusema kabla, ili kuwasaidia watu ambao tayari wameshaamua kuwa na Lowassa na pengine kumpigia kura kutokana na ushawishi wa kampeni zinazoendelea, na hivyo hotuba yake hiyo kutokuwa ya msaada sana kwa wakati huu.
Kwa upande wa Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Alexander Makulilo, alisema uamuzi alioufanya Dk. Slaa ni haki ya kidemokrasia ya mtu kama sheria za nchi zinavyoeleza.
“Alichokifanya ni haki ya kidemokrasia kwa kuwa katiba ya nchi imeeleza mtu halazimishwi kuwa chama fulani bali ni utashi wake,” alisema Dk. Makulilo.
Aidha, alisema kitendo hicho hakina haja ya kupingwa kwa kuwa watu wengi ni wafuasi na siyo wanachama.
Naye Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam, Idara ya Mawasiliano, Danford Kitwana, alisema amesikitishwa na kitendo cha Dk. Slaa ambaye anaamimika kuwa na dhamira ya kulikomboa taifa na kuliletea mabadiliko baada ya kusema Chadema kimaadili kibaya kuliko chama tawala.
Kitwana alisema hana tatizo na mtazamo alioutoa Dk. Slaa, bali mashaka yanakuja kutokana na hotuba yake kuonyesha mafisadi wapo Chadema wakati inaaminika CCM ndicho chenye idadi kubwa ya mafisadi.
Profesa wa uchumi, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Tawi la Dar es Salaam, Prosper Ngowi, amesema kujiuzulu kwa Dk. Slaa kumetokana na upeo na mtazamo alionao kiongozi huyo katika kutazama mambo.
Prof. Ngowi alisema uamuzi wa kujiweka pembeni na siasa ya vyama au kushiriki ni hiari ya mtu hailazimishwi.

Saturday, July 11, 2015

PICHA ZA KINACHOENDELEA DODOMA, MAKAO MAKUU YA CCM MUDA HUU..!!

DSC_2734
Kikao cha Halmashauri Kuu kimeendelea sasa hivi kwa zaidi ya saa nne hapa Makao Makuu ya CCM Dodoma, viko vitu vingi  vinaendelea nje ya Ukumbi… wapo wanaoimba na kushangilia, wengine wapo wakiendelea kusubiri kile kitakachotangazwa baada ya Halmashauri Kuu kumaliza Kikao.
Watu ni wengi sana nje ya Ukumbi, nimebahatika kukutana na wenyeji wa Mji wa Dodoma na watu ambao wanafanya shughuli zao kwenye Majengo yanayozunguka Makao Makuu hayo, wanasema haikuwahi kutokea mtaa huu ukawa busy watu wakawa wengi kiasi hiki.
DSC_2702
Hapa ni nje ya Ukumbi ambao Kikao kinaendelea.
DSC_2739
Baadhi ya Wajumbe wakiwa nje ya Ukumbi.
DSC_2741
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa nje ya Ukumbi pia.
DSC_2751
DSC_2760
DSC_2762
Waziri Lukuvi akitembea kuelekea Ukumbini.
DSC_2770
.
Hawa ilikuwa bahati mbaya wakapata ajali jirani na gari la Polisi.
DSC_2782
Huyu alionekana kwenye vurugu nje ya Ukumbi, Polisi wakamchukua.
DSC_2785
Gari nyingi za Polisi na FFU zimezunguka Ukumbi kuhakikisha Usalama upo wakati wote.
DSC_2798
Wanaoshangilia hawajachagua pa kukaa, ni mchana jua kali lakini wapo hapa wakati wote.
DSC_2806
Kila mtu kaaangalia panapomfaa, wengine wako juu ya ukuta.
DSC_2814
Akina mama na wadada nao hawajaogopa kusimama juu ya ukuta.
DSC_2819
DSC_2829 DSC_2831 DSC_2834 DSC_2837 DSC_2841 DSC_2856 DSC_2859 DSC_2861

KUTOKA DODOMA,, HAWA NDIO WAGOMBEA WATANO WALIOTAJWA NA CCM..!!

CCM
July 10 2015 inaripotiwa taarifa nyingine kutoka Dodoma Tanzania… Watu wengi wamekaa tayari kujua nini ambacho kitaamriwa Dodoma kuhusu Mgombea Urais ambae anateuliwa na CCM kugombea Urais wa Tanzania 2015.
Majina yalikuwa mengi zaidi ya 38, hii ndio list ambayo imetangazwa kuingia Top Five kupitia ukurasa wa Twitter wa CCM @ccm_tanzania
CCM II

Sunday, June 14, 2015

NA HII NDIYO LIST YA WASHINDI WOTE WA TUZO ZA KTMA..


Bendi Bora ya Mwaka - FM Academia

Wimbo bora wa kushirikiana/kushirikishwa - MwanaFA ft. Ali Kiba - Kiboko Yangu

Msanii Bora Chipukizi Anayechipukia - Barakah Da Prince

Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Tanzania - Waite - Mrisho Mpoto

Wimbo bora wa Zouk/Rhumba - Ntampata Wapi - Diamond Platnumz

Wimbo bora wa Afro-Pop - Mwana - Ali Kiba

Video ya bora ya muziki ya Mwaka - Mdogo Mdogo - Diamond Platnumz

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka bendi - Amoroso

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka Bongo Flava - Nahreel

Mtunzi bora wa mwaka Hip Hop - JohMakini

Mtunzi bora wa mwaka bendi - Jose Mara

Mtunzi bora wa mwaka Bongo Flava - Ali Kiba

Mtunzi Bora wa mwaka Taarab - Mzee Yusuf

Wimbo Bora wa Afrika Mashariki - Sura Yako - SautiSol

Msanii Bora wa Hip Hop - JohMakini

Rapper bora wa mwaka bendi - Ferguson

Wimbo bora wa reggae/dancehall - Maua Sama

Wimbo bora wa Hip Hop - Kipi Sijasikia - Prof Jay ft. Diamond Platnumz

Wimbo Bora wa R&B - Sisikii - Jux

Wimbo Bora wa Kiswahili Bendi - Wale Wale - FM Academia

Wimbo Bora wa Mwaka - Mwana - Ali Kiba

Wimbo bora wa Taarab - Mapenzi Hayana Dhamana - Isha Mashauzi

Muimbaji Bora wa Kiume Bendi - Jose Mara

Mwimbaji Bora wa kike Taarab - Isha Mashauzi

Mwimbaji Bora wa Kiume Taarab - Mzee Yusuf

Muimbaji Bora wa Kike Bongo Flava - Vanessa Mdee

Muimbaji Bora wa Kiume Bongo Flava - Ali Kiba

Mtumbuizaji bora wa muziki wa mwaka wa kike - Vanessa Mdee

Mtumbuizaji bora wa muziki wa mwaka wa kiume - Ali Kiba

HIZI NI BAADHI YA PICHA ZA TUKIO ZIMA LA KILI MUSIC AWARDS..

June 13 2015 katika ukumbi wa  Mlimani City Dar, Ndipo ilipofanyika KTMA. washindi wametajwa na kukabidhiwa Tuzo zao.. Hapa kuna picha zao zote kutoka kwa Milllard Ayo, unaweza kucheki kuanzia mwanzo mpaka mwisho tukio lilivyokuwa..

DSC_2350
DSC_2353
DSC_2390
DSC_2396
DSC_2408
DSC_2422
DSC_2442
DSC_2525
DSC_2533
DSC_2551
DSC_2587
DSC_2638
DSC_2728
DSC_2759
DSC_2772
DSC_2791
DSC_2811
DSC_2880
DSC_2930
DSC_2944
DSC_2997
DSC_3054