Blogger Widgets

Friday, August 30, 2013

Na hii ndio hatua ya makundi UEFA!!!


DIAMOND AMSHANGAZA MZEE GURUMO!!

Msanii  wa muziki wa kizazi kipya nchini, Maaruf kama Diiiamond Platnumz, Aliwaacha watu midomo wazi katika uzinduzi wa video yake mpya, Baada ya kumzawadia Mzee Gurumo, mwanamuziki wa miaka mingi na mkongwe aliyetangaza kustaafu mziki siku chache zilizopita zawadi ya Gari aina ya "Fun Cargo"


Tukio hilo limetokea usiku huu ndani ya ukumbi wa SERNA HOTELkatikati ja jiji la DSM ambapo Diamond Platnum anazindua video yake mpya huku Kiingilio cha show hiyo ikiwa ni bureeeeeeeeeeeee...






Thursday, August 29, 2013

DAH! 'BEEF' YA KAGAME NA RAIS WA TANZANIA IMEFIKIA HAPA!!!

RAIS Paul Kagame wa Rwanda, sasa hayupo tayari kukanyaga ardhi ya Tanzania kutokana na kile kinachoonekana kuwa ni mgogoro wa kidiplomasia unaoendelea kati yake na Rais Jakaya Kikwete.

Wakati hayo yakifikia hapo, kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (EALA), linakoketi mjini Arusha kilivunjika baada ya Spika wa bunge hilo, Magreth Zziwa, kugongana kauli na Mbunge mmoja wa Rwanda jambo lililosababisha wabunge wote wa Rwanda kususia kikao na kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.

Mwenendo wa hayo yaliyojitokeza jana katika Bunge la Afrika Mashariki hadi kikao kuvunjika, msingi wake ni mgogoro unaowagusa wakuu hao wawili wa dola.

Habari zilizolifikia gazeti hili toka katika vyanzo vyake mbalimbali vilivyo ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, lakini pia katika vikao vya Bunge hilo la Afrika Mashariki vinavyoendelea jijini Arusha zinaeleza kuwa, Rais Kagame hata kama ataalikwa kuja nchini leo, hatakuja.

MTANZANIA Jumatano limedokezwa kuwa jambo hilo tayari limethibitishwa na Wabunge wa Rwanda wanaohudhuria vikao vya (EALA).

Taarifa toka ndani ya Bunge hilo zilizolifikia MTANZANIA Jumatano zinaeleza kuwa, tayari mzimu wa msigano huo uliojitokeza baina ya wakuu hao wawili wa dola, umeanza kuwavuruga wabunge hao baada ya jana kikao cha Bunge hilo kuvunjika, kutokana na kuibuliwa kwa hoja ya kutaka vikao vya Bunge hilo kufanyika kwa utaratibu wa kuzunguka kila nchi.

Zinaeleza zaidi kuwa; Ni katika hoja hiyo wabunge wa Kenya na Rwanda walionekana kuungana na kuwa kitu kimoja na hivyo kususia kikao hicho cha jana, jambo ambalo lilimlazimisha Spika wa Bunge hilo, Magreth Zziwa kuvunja kikao.

Monday, August 26, 2013

YALIYOMO kwenye MAGAZETI YA LEO, Monday, August 26, 2013









SPORTS: Real Madrid and Tottenham have agreed a world record £86 million deal for Gareth Bale!


Spurs chairman Daniel Levy finally accepted the Spanish giants’ offer on Sunday and official confirmation of the transfer is expected in the next 48 hours.The clubs have come to an agreement on a straight cash deal to be paid in three installments, as Bale becomes the most expensive player in history, eclipsing the £80m Real paid Manchester United for.... >>Read More<<

Sunday, August 25, 2013

Mwenyekiti Freeman Mbowe na Viongozi wengine wa CHADEMA washikiliwa na Polisi Iringa!

Mwenyekiti Freeman Mbowe, wabunge Tundu Lissu, Peter Msigwa, Joseph Mbilinyi (Sugu), David Silinde na viongozi wengine wa mkoa na Wilaya ya Iringa mjini, akiwemo Diwani Nyalusi, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu Iringa, kwa kosa la kuzidisha muda wa mkutano.

Polisi wanasema mkutano ulimalizika saa 12.30 badala ya saa 12.00

Source: Jamii Forums 

Swali lwa msingi kwa Polisi, sheria gani wanayotumia katika suala hili. Au ni ule mwendelezo wa kutumiwa na kutumiwa na kutumiwa na kutumiwa.

Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Jeshi la Polisi, zote hazizungumzii muda specific wa kufunga mkutano, bali sun set. Kwa sababu sun set inategemea geographical location. Maeneo kama Kigoma saa 1 jioni, jua linawaka kama vile saa 12.

Ni Sheria ya Uchaguzi pekee, ndiyo inazungumzia muda maalum ambao ni 12.30. Na ni kwa sababu ya mazingira ya equality kwa ajili ya wagombea wote kufanya kampeni ndani ya muda mmoja.

Thursday, August 22, 2013

YALIYOMO KWENYE MAGAZETI YA LEO,, Thursday, August 22, 2013










Tuesday, August 20, 2013

PICHA: Hivi ndivyo hali ilivyokuwa Jijini Mwanza Jana!!













Monday, August 19, 2013

HIVI NDIVYO YULE TRAFIK FEKI ALIVYOANZA KAZI!!!


SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari 'feki' wa Usalama Barabarani mwenye cheo cha Sajini, akifanya kazi ya kuongoza magari eneo ya Tabata Kinyerezi, Dar es Salaam, mambo mapya yamezidi kubainika juu ya sababu za mtu huyo kujiingiza katika kazi hiyo bila kutambuliwa na Jeshi la Polisi.
Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vya kuaminika, zinasema trafiki huyo 'feki', ambaye inadaiwa jina lake halisi ni James Juma Hussein (45), mkazi wa Kimara Matangini, alianzia kazi hiyo mkoani Singida kabla ya kujipa uhamisho wa kikazi kwenda Dar es Salaam..

Sunday, August 18, 2013

Waislamu Msikiti wa Mtambani ‘Wamteka’ Askari Polisi!!

BAADHI ya waumini wa Kiislamu Msikiti wa Mtambani Jijini Dar es Salaam jana wamemkamata mmoja wa askari wa Jeshi la Polisi na kumshikilia kwa muda kabla ya kumwachia kwa masharti kadhaa. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi kimebainisha askari aliyekamatwa ni Jonathan Tossi ambaye anafanya kazi kitengo cha habari na uhusiano wa Jeshi la Polisi.
Polisi wakizunguka eneo la Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam kuhakikisha kuna amani.

Askari huyo alijikuta akiingia kwenye mikono ya waumini hao alipokuwa akitekeleza majukumu yake (kazini) akipiga picha mtaani maeneo ya Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam. Taarifa zaidi zinasema baada ya waumini hao kumkamata askari huyo walimuhoji kwa muda kisha kutaka kitambulisho chake na kumuamuru afute picha zote alizokuwa akipiga eneo hilo ili wamuachilie kwa usalama wake.
“Kutokana na kuhofia usalama wake alikubaliana nao na kisha kufta picha zote alizopiga. Walimtaka pia aoneshe kitambulisho na kuhoji ni kwanini anapiga picha wakati yeye ni askari…baada ya kukubaliana na masharti hayo walimuachia,” kilisema chanzo chetu.
“Sisi wenyewe tunashangaa wapiga picha walikuwa wengi wa vyombo mbalimbali vya habari hatujui hawa walijuaje kwamba yule jamaa alikuwa askari na wakati alikuwa amevaa kiraia,” alisema shuhuda mmoja aliyekuwa eneo la tukio.
Leo mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ulinzi na doria iliim*rishwa na Jeshi la Polisi ambapo magari na pikipiki za Polisi zikiwa na askari waliojiandaa kutuliza ghasia yalikuwa yakizunguka ikiwa ni kujiandaa kwa kukabiliana na vurugu zozote.
Mitaa kadhaa mwandishi wa mtandao huu alishuhudia askari walio na mabomu ya machozi, huku wakiwa wamevalia vifaa maalumu vya kujikinga na risasi wakizunguka kwenye magari yao maeneo mbalimbali likiwemo eneo la Msikiti wa Mtambani Kinondoni jijini Da rs Salaam. Hata hivyo hakuna taarifa za kutokea vurugu zozote.
Taarifa ambazo hazikuthibitishwa zinasema doria ya polisi ililazimika kufanywa baada za kuwepo na taarifa kuwa huenda wafuasi wa Shekhe Issa Ponda wangelifanya fujo kutokana na kutoridhishwa na hatua ya kukamatwa kwa kiongozi huyo kwa tuhuma kadhaa zinazomkabili.
Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, kuzungumzia kwa kina taarifa hizi hazikuzaa matuna. Hata hivyo Thehabari inaendelea kumtafuta kwa ufafanuzi zaidi wa tukio la kukamatwa kwa askari wao na kuachiwa.

MWAKYEMBE AWAANIKA WALIOMSAIDIA MASOGANGE KUPITISHA DAWA ZA KULEVYA AIRPORT!!!

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe jana ameanika majina ya watu saba waliohusika kupitisha mabegi tisa yaliyokuwa na kilo 180 za dawa za kulevya zenye thamani ya Sh8 bilioni, Julai 5 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wakiwamo maofisa usalama wanne wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na polisi mmoja.


Alisema mizigo ikishaondoka mikononi mwa abiria hukaguliwa tena kwa kutumia mbwa wa Idara ya Usalama wa Taifa, lakini siku ya tukio hilo mbwa hao walichelewa na walitumika baada ya mizigo kuingizwa kwenye masanduku ya chuma.
“Kwa abiria watatu kuwa na mabegi makubwa tisa yanayofanana si kitu cha kawaida kukwepa jicho la maofisa wa ushuru wa forodha na vyombo vya usalama, sijui walikuwa wapi siku hiyo?” alihoji Mwakyembe.
Juzi waziri huyo aliahidi kuyaweka hadharani majina ya watu wanaosafirisha dawa za kulevya nchini, na alitekeleza ahadi hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari, kusema kuwa watu hao wamenaswa baada ya mfumo wa kamera (CCTV) za uwanja huo kudaka matukio kadhaa yaliyotokea siku ya tukio hilo, kuanzia saa 9:25 hadi saa 10:30 alfajiri.
Ameagiza wafanyakazi hao wanne pamoja na askari polisi mwenye cheo cha koplo, mbeba mizigo na mfanyabiashara aliyekuwa na wasichana wawili waliokamatwa Afrika Kusini, (ambao hatuwezi kuwataja kutokana na kushindwa kuwapata kujieleza) kuchukuliwa hatua za kinidhamu, kukamatwa na kuunganishwa na watuhumiwa waliokwenda na mzigo huo Afrika Kusini.
Mabegi hayo yaliyokuwa na dawa za kulevya aina ya ‘Crystal Methamphetamine’, yalipitishwa na wasichana wawili wasanii aliowataja kuwa ni Agnes Gerald ‘Masogange’ na Melisa Edward ambao walidakwa siku hiyohiyo katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, Afrika Kusini na tayari wameshafikishwa mahakamani.
Juzi Dk Mwakyembe alifanya ziara JNIA kukagua utendaji kazi kwenye uwanja huo ikiwa ni siku tatu baada ya ahadi aliyotoa akiwa Mwanza kwamba katika kipindi cha wiki mbili, atahakikisha anawakamata vigogo wote walio katika mtandao wa usafirishaji na uingizaji wa dawa za kulevya kupitia viwanja vyote vya ndege nchini.
Saa nane baada ya ziara hiyo, Maofisa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wanadaiwa kumkamata Edwin Monyo akiwa na kete 86 za dawa aina ya heroini na misokoto 34 ya bangi aliyokuwa akiisafirisha kwenda Italia kupitia Zurich.
Mpango ulivyosukwa
Alisema siku ya tukio saa 9:28 kamera hizo za usalama zilimwonyesha mbeba mizigo wa uwanja huo akiwa anazungukazunguka eneo la kuingilia abiria kama mtu ambaye ana ahadi na kukutana na mtu fulani.
“Kamera pia zilimnasa ofisa mwingine wa TAA kwa mara kadhaa akitoka na kuingia ndani ya jengo la abiria huku akizungumza na simu, kitendo ambacho hakiruhusiwi kabisa kwa wafanyakazi wa eneo la ukaguzi wa abiria,” alisema na kuongeza;
“Wakati huohuo, kamera zilikuwa zinamwonyesha askari polisi anayetuhumiwa kuhusika katika mpango huo akiwa anarandaranda eneo la uhakiki wa hati za kusafiria kama vile anasubiri kitu fulani.”

Wednesday, August 7, 2013

Mfanyabiashara Maarufu wa Madini Auwawa kwa kupigwa Risasi Arusha!!

ARUSHA: Mfanyabiashara maarufu wa madini Mererani na Mmiliki wa SG RESORT ya Arusha, Bw. Erasto Msuya ameuwawa leo majira ya alasiri wakati alipokuwa akitokea Mererani kuelekea Moshi. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimepatikana mara baada ya tukio hilo zinasema kuwa mfanyabiashara huyo alipigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi mara baada ya majibizano ya risasi yaliyotokea maeneo ya barabara ya kia. inasemekana wauaji wamekimbia na briefcase yake.



Monday, August 5, 2013

WANAFUNZI 8000 WAKWAMA KUJIUNGA VYUO VIKUU NCHINI!!!

TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imekataa majina ya wanafunzi 8,805 walioomba kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza katika taasisi za elimu ya juu nchini kwa mwaka wa masomo 2013/2014 kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza kwenye fomu za waombaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa TCU
 Profesa Sifuni Mchome, wanafunzi hao hawakuchaguliwa na tume hiyo kujiunga na vyuo vikuu kutokana na maombi yao ya programu zote walizochagua kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa sababu za kutochaguliwa kwa wanafunzi hao ni pamoja na ushindani wa wanafunzi katika programu walizochagua, wanafunzi kushindwa kuwasilisha programu walizochagua na kuchagua programu ambazo hawana sifa nazo.
Hata hivyo, TCU imesema inawapa nafasi nyingine wanafunzi hao kuomba tena kwa awamu ya pili kwa kuchagua programu nyingine ambazo wana sifa nazo kupitia mfumo wa udahili wa TCU, ambao umeshafunguliwa tangu Julai 29 hadi Agosti 9, mwaka huu, utakapofungwa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwanafunzi anatakiwa kuangalia jina lake katika orodha ya wanafunzi ambao hawakuchaguliwa na TCU, orodha inayopatikana kwenye tovuti ya taasisi hiyo.
"Ba a d a y a mwa n a f u n z i kuthibitisha jina lake kwenye orodha ya wanafunzi ambao hawakuchaguliwa iliyoko kwenye tovuti ya TCU, unatakiwa kufuata masharti yafuatayo, chagua programu moja tu kutoka kwenye orodha ya programu inayopatikana kwenye tovuti ya TCU," ilisisitiza taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa masharti hayo, pia mwanafunzi anatakiwa kufungua mwongozo wa udahili unaopatikana kwenye tovuti hiyo na kuthibitisha kwamba anayo sifa stahiki ya kujiunga na programu aliyoichagua.

Jaji Francis S.K. Mutungi ateuliwa kuwa msajili wa vyama vya siasa!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K. Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Taarifa iliyotolewa Dar Es Salaam leo, Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.

Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.

Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.

Imetolewa na: 
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, DAR ES SALAAM.