Blogger Widgets

Thursday, September 25, 2014

Msikilize hapa T.I na alichokisema kuhusu kuja Bongo..!

T.I 3Kupitia XXL ya CloudsFM September 23 2014 ndio T.I ametangazwa kuwa staa wa muziki wa kimataifa ambae atakua mgeni kwenye stage ya Fiesta 2014 Leaders Club KinondoniOctober 18.
T.I ni rapper kutokea Atlanta Georgia Marekani na umri wake ni miaka 33 na ni mkali wa hiphop duniani ambae ujazo wa jina lake ulianza kuonekana mwaka 2003 pale aliposhirikishwa na Bone Crusher kwenye single ya ‘never scared
T.I 2

Huu ndio Mchongo alioupata Diamond Kwenye App Mpya ya "Mziiki"

Diamond PlatinumzIngawa hajaweka wazi namna dili hii itakavyokuwa lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram,Diamond Platnumz amepost picha ambayo imebeba maandishi yasemayo ‘Ningependa kukutaarifu shabiki wangu pendwa kuwa kijana wako sasa ni balozi wa application mpya iitwayo Mziiki’.
Hii ni application ambayo itatumiwa na watu wenye simu za androad kusikiliza muziki huu ndiyo muonekano wake utakapokuwa ume instal kwenye simu yako.
mond3
Maandishi ya Diamond pamoja na alichokipost ni hiki.
mond
mond 2

Monday, September 15, 2014

BRAND NEW: KUTOKA KWA PROFFESOR JAY, HIZI NDIO VIDEO MBILI ALIZOZIACHIA KWA PAMOJA..!


Rapper mkongwe  Joseph Haule aka Professor Jay usiku wa Jumamosi (13 Sept) alizindua video mbili ‘Kipi Sijasikia &  ‘3 Chafu’,uzinduzi huo ulifanyika ndani ya ukumbi wa Ten Lounge uliopo maeneo ya Victoria jijini Dar es Salaam
Mbali na uzinduzi huo Professor alipata support kutoka kwa wasanii mbalimbali  akiwemo,Linex,Chid Benz,Lady Jay Dee,Soggy Doggy,TID,Slim,D Knob,Country Boy na wengineo..
Video zenyewe ndio hizi hapa, zitazame na utoe maoni yako..



Na video ya pili ni hii ya Tatu chafu.. itazame hapa..

Wednesday, September 10, 2014

ULIONA HII? HIZI NDIO PRODUCTS MPYA KUTOKA APPLE

news newsNajua kuna uwezekano ukawa ulisikia fununu sana kuhusu iPhone6 au hata kuona baadhi ya taarifa feki kuhusu simu hii mpya, post hii ni maalum kukuletea taarifa sahihi na ya ukweli kuhusu iPhone6 ambayo ndio imetambulishwa rasmi.
Wanasema simu zote hizi mbili mpya zina A8 processor ambayo inafanya ziwe na kasi zaidi kuliko iPhone5 kwa asilimia 20.
iphone 6 1
Unaambiwa zote iPhone6 na iPhone6 plus zimekuja na screen kubwa tofauti na nyingine zilizotangulia
iphone 6 2
Apple wenyewe wanasema simu hizi mbili za iPhone6 na iPhone 6 plus zina 8 megapixel camera ambayo itasaidia camera kupata focus faster.
iphone 6 3
Simu hizi zote mbili zitaanza kupatikana nchini Marekani September 19 2014 nchini Marekani pamoja na kwenye nchi nyingine nane duniani.
iphone 6 4
Simu hizi za iPhone 6 na iPhone 6 pluz zitaambatana na saa hii ambayo unaweza kuitumia kufanya mambo mbalimbali ambayo yapo kwenye simu pia
iphone 6 5
Apple wanasema malengo yao ni k’uireplace’ au kuichukua nafasi ya Wallet, yani kurahisisha mambo kwenye iPhone kiasi kwamba hutohitaji kutembea na wallet.
Mengine yaliyosemwa ni pamoja na >>  ‘the bigger displays allow for bigger batteries: 11 hours of video watching on the iPhone 6 and 14 hours for the iPhone 6 Plus — up from 10 hours on the iPhone 5S
And the iPhones will come with Apple’s new iOS 8 software, featuring a new HealthKit application that monitors users’ heart rates, sleep, weight and blood pressure among other health-related information. Apple said iOS 8 will be available Sept. 17 to customers who have an iPhone 4S, iPhone 5, iPhone 5C or iPhone 5S.
iphone 6
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

HIVI NDIVYO KIFARU CHA JESHI LA WANANCHI (JWTZ) KILIVYOUA HUKO LINDI..!!

kifalu


Kutoka Lindi kuna taarifa ambayo imethibitishwa pia na kamanda Mpinga kuhusu ajali iliyotokea Mtwara ambayo imehusisha gari la Jeshi la Wananchi Tanzania(Jwtz)imeripotiwa asubuhi ya leo na shuhuda wa eneo hilo.
Msafara huo wa Wanajeshi ulikuwa ukitokea Mtwara kuelekea Nachingwea kwenye camp kubwa ya Jeshi na ajali hiyo imetokea maeneo ya Mnolela kijijini Lindi,kwa mujibu wa shuhuda ambaye ametoa taarifa hii kupitia kipindi cha Power Breakfast kutoka Clouds Fm amesema ajali hiyo imeua wanajeshi 3 na mwenye nyumba mmoja ambaye ni mwanamke alikua kalala ndani. Kifaru hicho kilikosa mwelekeo katika eneo lenye kona kali na kugonga nyumba iliyokuwa kando ya barabara na kisha kutoka na kuivaa nyumba nyingine ya pili. 
Madhara mengine yaliyotokana na ajali hii ni nyumba mbili kuharibika vibaya,majeruhi wa ajali hii wamepelekwa kwenye hospital ya Mkoa wa Mtwara.

Tuesday, September 9, 2014

BRAND NEW AUDIO: KUTOKA KWA JUX,, TRACK NYINGINE KALII HII DOWNLOAD HAPA..

Baada ya ile ya Uzuri wako na Nitasubiri kufanya vyema katika soko la bongo fleva, sasa track nyingine kali na mpya kutoka kwa Jux ndio hii hapa.. Wimbo unaitwa Sisikii, ambao ni Production ya Bob Maneck toaka A.M Records..
Sikiliza na Download hapa..


Kutoka kwa Prince Dully Sykes,, Hii ndio video yake Mpya iliyotengenezwa na Adam Juma..

Screen Shot 2014-09-09 at 10.44.16 AMDirector wa video Adam Juma ni miongoni mwa watu waliopewa heshima kwa kuleta mabadiliko makubwa kwenye bongofleva ambapo mkono wake umeonekana kwenye video nyingi za bongofleva ambazo zimefikia kuchezwa hata na baadhi ya vituo vikubwa vya TV Afrika.
Time hii Adam ameuweka mkono wake kwenye video mpya ya Dully Sykes ‘togola’ ambayo ndio hii hapa chini, unaweza kuitazama..

Monday, September 1, 2014

IKIWA LEO NDIO MWISHO WA USAJILI ULAYA,, HUYU NDIO NYOTA ALIYESAJILIWA NA MAN UTD LEO..!!!

IMG_6909.PNG
Leo ndio siku ya mwisho ya usajili barani ulaya na kila klabu ipo katika harakati za kuimarisha timu zao.
Klabu ya Manchester United leo hii imezishinda Manchester City, Real Madrid, Arsenal katika mbio za kusaka saini ya mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia Radamel Falcao.
United ambayo juzi ilikamilisha usajili wa Angel Di maria, leo imekamilisha usajili wa Falcao kwa mkataba wa mkopo wa mwaka 1 ambao una gharama ya £12m.
Falcao anategemea kutua jijini Manchester leo jioni kwa ajili ya vipimo vya afya na kusaini mkataba.

NECTA KUANZA KUTOA MATOKEO KWA MFUMO WA GPA..

BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA), limetangaza mfumo mpya wa upangaji wa madaraja ya ufaulu kwa kutumia wastani wa pointi (GPA) ambao utaanza kutumika katika mtihani wa kidato cha nne 2014 na cha sita 2015.

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde, alisema kuwa mfumo huo umekuwa ukitumika katika kupanga madaraja ya ufaulu katika baadhi ya mitihani inayosimamiwa na baraza hilo.

Alisema manufaa yake ni kuwa na mfumo wa kutunuku matokeo wa ina moja katika ngazi zote za mafunzo kuanzia elimu ya msingi hadi elimu ya juu; matokeo yaliyo katika mfumo huo kwenye cheti yatarahisisha kazi ya udahili wa watahiniwa unaofanywa na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na NACTE katika ngazi za juu za mafunzo.

Pia aliongeza kuwa mfumo wa GPA ni rahisi kuelewa kwa wadau wa kada mbalimbali kwa sababu hutoa tafsiri yenye kuonesha mtahiniwa aliye na GPA kubwa ndiye aliye na maokeo mazuri.

Kwa mujibu wa Dk. Msonde, madaraja katika mfumo wa GPA hupangwa katika utaratibu wa Distinction, Merit, Credit na Pass ambapo daraja la juu ufaulu ni Distinction na la chini ni Pass.

Kulingana na utaraibu huo, daraja la Distinction litakuwa na alama kati ya 3.6-5.0, Merit 2.6.3.5,Credit 1.6-2.5, Pass 0.3-1.5 na Fail 0.0-0.2 kwa matokeo ya kidato cha nne wakati wa kidato cha sita Distinction ni kati ya 3.7-5.0, Merit 3.0-3.6, Credit 1.7-2.9, Pass 0.7-1.6 na Fail 0.0-0.6.

“Ukokotoaji wa wastani wa pointi (GPA) ya mtahiniwa hufanywa kwa kuzingatia masomo ambayo mtahiniwa amefaulu. GPA anayopata mtahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne hutokana na wastani wa pointi alizopata katika masomo saba aliyofaulu vizuri wakati kwa kidato cha sita ni masomo matatu,”alisema.