Blogger Widgets

Sunday, May 5, 2013

UPDATES: Mlipuko wa bomu kanisa la Olasiti Arusha

Hadi sasa Jeshi la polisi linamshikilia mtu mmoja akihusishwa na mlipuko uliotokea katika kanisa la Katoliki Olasiti Arusha

Kwasasa majeruhi wanaripotiwa kuwa 30, ila watu watatu wameumia vibaya sana na hali zao sio nzuri.

RPC mkoa wa Arusha ametoa hotuba yake na kusema ni tukio la kigaidi, pia amesema wanawasaka wote waliohusika na tukio hilo na ameomba watanzania wawe watulivu wakati wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Uzinduzi wa kanisa hilo la Mtakatifu Joseph parokia ya Olasiti umesitishwa hadi hapo utakapotangazwa baadaye..


Picha zaidi juu ya tukio hilo:





Mkuu wa mkoa wa Arusha akielekea eneo la tukio

Baadhi ya Majeruhi wa tukio hilo





BREAKING NEWS! KANISA LALIPULIWA ARUSHA!!!

BREAKING NEWS!!

Mlipuko mkubwa umetokea katika kanisa Katoliki la Mt. Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti Arusha. Watu kadhaa wamejeruhiwa wakati wa ibada ya uzinduzi wa kanisa hilo iliyokuwa ikiongozwa na Balozi wa Papa nchini.
Haijajulikana kama ni bomu au la ila ni mlipuko mkubwa na watu wamejruhiwa..


Ukiwa Arusha tune FM 106.70

Nukuu kutoka Redio Maria 

....watu wengi wamejeruhiwa miguu

......ni mlipuko

.....Olasiti Arusha

...kitu kilirushwa au kutokea chini kwenye moramu iliyo mwagwa....

....kuna watu wanahisiwa kuja eneo la tukio kwa gari na kurusha hiko kitu na kukimbia kutokomea na gari...maelezo ya mtoto mdogo anaye sadikiwa kuona watuhumiwa....

...watoto wengi na kina mama wamejeruhiwa....


Stay with us for more updates..

Friday, May 3, 2013

CCM WAMJIA JUU MKUU WA MKOA ARUSHA.. Wadai amemwongezea umaarufu Lema


• WADAI AMEMWONGEZEA UMAARUFU LEMA, CHADEMA

Mkuu wa Mkoa Arusha, Ndg. Magesa Mulongo



VIGOGO wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwemo wabunge, wamemjia juu Mkuu wa Mkoa (RC) wa Arusha, Magessa Mulongo kwa jinsi alivyoshughulikia kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).

Wabunge hao walikiambia chanzo hiki mjini Dodoma kuwa kesi ya uchochezi iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Lema kwa shinikizo la mkuu huyo... >>Read More>>>