Blogger Widgets

Friday, October 24, 2014

UMESIKIA HII YA BOKO HARAM KUTEKA WANAWAKE WENGINE? HEBU CHEKI NAYO HAPA..

Nigeria Kidnapped GirlsTaarifa iliyoripotiwa na shirika la utangazaji Uingereza BBC imesema kikundi cha wapiganaji cha Boko Haram kimefanya mashambulizi katika kijiji cha Adamawa kilichopo Kaskazini Magharibi ya Nigeria na kuteka wanawake na wasichana katika kijiji hicho.
Utekaji wa wasichana na wanawake hao unatokea ndani ya siku sita tangu serikali ya Nigeria na kikundi hicho walipofanya makubaliano ambapo Boko Haram waliahidi kuwaachilia huru zaidi ya wasichana 200 wanaoshikiliwa na kikundi hicho.
Japo Boko Haram wamekiuka makubaliano waliyoafikiana Ijumaa iliyopita, bado serikali ya Nigeria ina matumaini ya kuachiliwa huru kwa wasichana hao baada ya kikao kinachotarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa huko Chad.

BRAND NEW: UMEISIKIA HII COLABO YA FA NA ALI KIBA? PITA NAYO HAPA..!

MwanaFAMwanaFA ambae hivi karibuni alitajwa na producer maarufu Hermy B kama Mkali miongoni mwa wachache bongoflevani wenye uwezo mkubwa wa kuandika pia mashairi, ameungana na Ali Kiba kuziteka headlines za bongofleva kwa single yao ambayo unaweza kuipakua hapa kupitia mkito.com

Wimbo ni wa mwana FA akiwa amemshirikisha Ali Kiba, na unaitwa Kiboko Yangu..
mkito.com ni tovuti mpya iliyo chini ya vijana walioamua kuwa serious kuongeza vipato vya Wasanii wa Tanzania hivyo kila unaposupport kwa kudownload au kusikiliza hii single ndivyo unaongeza kipato cha wakali hawa.
Au unaweza kuibonyeza hapa kupelekwa moja kwa moja kuipata >>> HAPA

UMEIPATA HII YA CHID BENZ KUKAMATWA NA POLISI AIRPORT? ICHEKI HAPA..

Najua kama umekua karibu na simu yako leo mitandao ya kijamii hasa Whatsap na twitter inaweza kuwa imetumika kukufikishia Taarifa zilizoanza kuzungumziwa na watu mbalimbali saa kadhaa zilizopita kwamba msanii Chid Benz amekamatwa na Polisi.
Taarifa zinasema kakamatwa na Polisi kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam akiwa anaelekea Mbeya na hiyo imetokea baada ya kukutwa na vitu ambavyo ni kosa kwa yeyote kukutwa navyo.
Wakati millardayo.com inaendelea kufatilia hii taarifa kwa upande wa pili wa Polisi, tumezungumza na muandaaji wa show ya Instagram Party ambayo Chid Benz ndio alikua anakwenda kushiriki kesho.
Chidi 1Fred amekiri kweli Chid Benz amezuiliwa na Polisi kwa kukutwa na vitu ambavyo hajavifahamu >>> “Sijapewa taarifa kamili lakini naambiwa kuna tatizo limetokea airport ya Dar es Salaam akiwa anasafiri kuja Mbeya, wameniambia kuna vitu ambavyo amebeba haviruhusiwi kupita Airport
Chidi Benz alikua ameongozana na msanii mwenzake ambae ni Shetta hivyo Chidi kabaki na Polisi na Shetta amekwenda kupanda ndege kwa ajili ya kuelekea Mbeya.

Monday, October 20, 2014

HAYA NDIO DIAMOND NA UONGOZI WAKE WALIYOZUNGUMZA BAADA YA FIESTA KUWAENDEA VIBAYA..!!

dmnOctober 18 ilikua ni siku maalum ya Wakazi wa Dar es salaam kula bata kwenye msimu wa mafanikio ambao unapita mara moja kila mwaka kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Ilikua ni good time ya ukweli sana Watanzania kumuona T.I kumuona Davido kumuona Victoria Kimani na Waje pamoja na wasanii wengine wa kimataifa ambao nao walihudhuria tamasha hili lililokuwa na watazamaji zaidi ya elfu hamsini.
Miongoni mwa wasanii waliopokelewa vizuri kwenye show hii ni pamoja na Mr Blue na Micharazo,Ally Kiba,Weusi,Vanessa Mdee,Stamina pamoja na Diamond Platnumz ambaye aliimba single 4 kwenye jukwaa hili.
Mashabiki wengi wa Ally Kiba inasemekana walipanga kuzomea wakati Diamond Platnumz anaperfoam pale jukwaani,kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm meneja wa Diamond Platnumz aitwae Babu Tale kaongelea hali hii.
taleHizi ni sentensi 10 alizozisema.
1.Sisi tumechukulia  sehemu ya mashindano,uzuri sisi tuliambiwa na uongozi wa Clouds kabla ya Diamond hajapanda ilikua saa 3 kamili tukaitwa tukaambiwa kuna watu wamejiandaa kumzomea Diamond.
2.Kama uongozi tulikaa na msanii wetu na kumjenga kisaikolojia na kumwambia kuna hivi vinatokea wao walitaka aanze Davido kisha afate Diamond kupunguza watu watakaozomea tukasema hapana pangeni show yenu kama ilivyokuwa ni sehemu ya mashabiki kufurahi.
3.Hatujaathirika kwamba msanii wetu ameshuka tunapoona watu wanapiga kelele kwa ajili yako au huna sifa ile unatakiwa uangalie umekosea wapi unaenda wapi,hatuna makosa kwa mashabiki wetu.
4.Kikubwa Diamond anafanya vizuri tunatakiwa kuhamisha macho yetu tumpigie kura Diamond kwenye tuzo za Channel  O Music Awards, kwa sababu mwisho wa siku chema chajiuza kibaya chajitembeza.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza 

Sunday, October 12, 2014

UMESIKIA KUHUSU HII FILAMU YA MAISHA YA LIONEL MESSI? Cheki Trailer ya Movie hiyo hapa..!!


Labda unapokuwa mtu maarufu duniani, unahitaji filamu itakayokuelezea maisha yako halisi, Lionel Messi kama mchezaji bora wa soka Duniani amefanikiwa kupata bahati hii ya kutengenezewa filamu.
Filamu hiyo iliyoongozwa na director Alex De La Iglesia, pamoja na kuhusisha maisha ya Messi pia imewahusisha marafiki na wanasoka wenzie Messi, kama vile Pep Guardiola, Pique, Pinto, Iniesta, na Mascherano, pia wachezaji wenzie wa timu ya Newell’s Old Boys.
Pamoja na kutokuwepo kwa Messi mwenyewe halisi, muongozaji filamu, Alex de le Iglasia amefanikiwa kuonyesha picha halisi ya maisha ya nahodha huyo wa Argentina.
Filamu hiyo ilizinduliwa jijini Rio de Janeiro na sasa inaonyeshwa kwenye kumbi za sinema huko Amerika ya kusini.
Tazama trailer ya Movie hiyo hapa..

Saturday, October 11, 2014

BRAND NEW: Ile Video ya Umebadilika kutoka kwa Young Killer na Banana Zoro si ndio hii hapa sasa..

Young Killer 67Kwenye mfululizo wa single zake alizowahi kutoa hii ni ya 5 ikiwa ni baada ya Dear Gambe,Jana na Leo,Mrs. SuperStar,My Power na hii inaitwa Umebadilika ambapo mwanzoni ilifanywa Classic Sound lakini ikaja kurudiwa na Combination Sound kwa Man Water.
Video imefanywa na Director Hefemi Mtanzania ambae anaishi na kufanya kazi nchini Marekani.

Thursday, October 9, 2014

BRAND NEW VIDEO: HIVI NDIVYO NAKAAYA ALIVYORUDI KWENYE GAME

Screen Shot 2014-10-09 at 10.37.45 AMNakaaya ni staa wa bongofleva ambae ujazo wa jina lake ulitokana na ‘Mr. Politician‘ ambapo baada ya hapo aliendeleza harakati zake kwenye huu muziki mpaka alipopata ajali Arusha ambayo ilimfanya awe kimya kwa muda mrefu.
Nakaaya ambae pia ni mama wa mtoto mmoja alietimiza mwaka mmoja siku chache zilizopita alirudi kwenye muziki baada ya kujifungua na kutoa single ya kwanza iitwayo ‘blessing‘ ambayo ni dedication pia kwa mwanae.
VIDEO IMEFANYWA NA CYNE STUDIOS ARUSHA.. Itazame hapa..


Wednesday, October 8, 2014

HII NDIO SABABU YA RAIS WA ZANZIBAR KUMFUKUZA KAZI MWANASHERIA MKUU, OTHMAN M. OTHMAN..!!

Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, amemfukuza kazi Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. OTHMAN MASOUD OTHMAN kwa kuvikataa baadhi ya vifungu vya rasimu ya Katiba.

Nini maoni yako kuhusu hili?

Photo: Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, amemfukuza kazi Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. OTHMAN MASOUD OTHMAN kwa kuvikataa baadhi ya vifungu vya rasimu ya Katiba.

Nini maoni yako kuhusu hili?