Blogger Widgets

Tuesday, April 29, 2014

Uliona hii? Cheki jinsi Beki wa Barcelona alivyokula ndizi aliyorushiwa na washabiki kama ishara ya ubaguzi wa rangi..!!

Mchezaji wa Barcelona, Dani Alves, juzi alitoa kali ya mwaka baada ya kula ndizi aliyotupiwa  na washabiki wa timu pinzani kama ishara ya ubaguzi wa rangi.. Tukio lilitokea juzi jumapili katika mchezo baina ya club ya Barcelona na Villareal.

Mchezaji huyo Raia wa Brazil alikuwa tayari kupiga kona mara ghafla ndizi iliyorushwa kutoka kwa washabiki ilitua mbele yake na kwa ujasiri aliokota ndizi hiyo, akaimenya na kuila kisha akapiga kona iliyozaa bao la ushindi kwa wababe hao wa spain...
Chekii video ya tukio hilo hapa...



Katika Mchezo huo Barcelona wallibuka na ushindi wa goli 3 dhidi ya 2 za wapinzani wao villareal.

Vitendo vya ubaguzi wa rangi vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara katika michezo hasa mpira wa miguu. Shabiki aliyebainika kufanya kitendo hicho ni wa Villareal na sasa anakabiliwa na adhabu ya kufungiwa maisha kuingia katika viwanja vya michezo na kunyang'anywa kadi ya uanachama wa club yake. Club ya Villareal iliomba radhi kutokana na tukio hilo.

Monday, April 28, 2014

Picha: Uliona Jinsi Jeshi la Wananchi lilivyozipamba sherehe za muungano? Cheki hapa!!

Uliskia hii?? Mashamba ya aliyekuwa gavana wa BOT, Daudi Balali kugawanywa kwa wananchi..!!

 Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Balali.
Kilombero. Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero imeamua kufuta miliki ya mashamba yote makubwa yasiyoendelezwa na taratibu mpya zinafanyika ili kuyamilikisha kwa wananchi.

Kati ya mashamba hayo, matatu ni ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Balali na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Klabu ya Simba, Marehemu Priva Mtema yaliyoko katika vijiji vya Lungungole na Merera ambayo wananchi wameshayavamia na kuendeleza shughuli za kilimo.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Kilombero juzi, Mwenyekiti wake, David Ligazio alisema taratibu za kuomba hatimiliki za mashamba hayo zifutwe zinaendelea.

Ligazio alisema wamiliki wa mashamba hayo wameshapewa notisi na orodha yao imeshawasilishwa kwa Kamishna wa Ardhi ili aridhie kufutwa kwa hati za mashamba hayo.

Alisema uamuzi wa kuyataifisha umekuja baada ya halmashauri kubaini kuwa yamekuwa hayaendelezwi na hivyo kusababisha maeneo hayo kuwa misitu wakati wananchi wanahitaji maeneo ya kulima.

Alisema ukaguzi wa kumbukumbu umeonyesha kuwa idadi kubwa ya wamiliki hao hawapo wilayani Kilombero na maeneo hayo yanamilikiwa kwa hati za muda mrefu bila kufuata taratibu.

Alisema utaratibu unaofanyika sasa ni kuwaagiza watendaji na wenyeviti wa vijiji, kuanisha ukubwa halisi wa mashamba hayo ili kurahisisha kazi ya kuyagawa kwa wananchi katika siku zijazo.

Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema taarifa hiyo haijafika ofisini kwake, lakini akabainisha kuwa kuna watu wengi wanaomiliki ardhi kubwa mkoani Morogoro bila kuwa na hatimiliki wala kufuata taratibu huku wakiwa wanawatisha wananchi.

Aliwataka wananchi hao kujisimamia, waondoe unyonge na kuzingatia taratibu za ardhi, kwamba inatakiwa kugawiwa kupitia mkutano mkuu wa kijiji, vinginevyo wana haki ya kujitwalia maeneo hayo na kufanya maendeleo mengine.

“Kuna matukio unakuta mtu anakaa na mwenyekiti wa kijiji na kujifungia, wanajadili wenyewe na kugawiana maeneo ya kijiji bila kuwashirikisha wananchi, hawa wananchi wanatakiwa kukataa hali hiyo,” alisema.

Maeneo yanayogawiwa

Mwenyekiti wa halmashauri aliyataja maeneo mashamba yanayotakiwa kugawanywa kwa wananchi na ukubwa wake katika mabano kuwa ni Lungongole (ekari 375) na Merea (ekari 373). Pia kuna shamba lenye ukubwa wa hekta 887 linalomilikiwa na Balali, ekari 491 zinazomilikiwa na George Teni katika Kijiji cha Kisegese na ekari 500 zinazomilikiwa na Aloyce Lyenga katika Kijiji cha Idete.
Katika orodha hiyo pia kuna ekari 30,000 za Kampuni ya Merera Plantation Ltd katika Kijiji cha Merera.

Mashamba mengine ni ekari 102 za Abdallah Sajiri zilizopo Kining’ina, ekari 295 za Peter Warwic zilizopo Lumemo, ekari 484.9 za Sadru Meghji zilizopo Msolwa Ujamaa, ekari 120 za Ranifa EC &DEV. Group zilizopo Kisegese na hekta 5,128 za Rubada zilizopo Ngalimila.
Ligazio alitaja mashamba mengine kuwa ni ekari 2,390 za kampuni iliyokuwa ya usafirishaji mkoani Morogoro zilizopo Mbingu, ekari 875 za Jerome Mwakifuna zilizopo Idete, ekari 656 za Priva Mtemanyanja zilizopo Lungongole na ekari 1,500 za Ngwasi River Valley Inv. zilizopo Mlimba.

Source >>Mwananchi<<

Sunday, April 27, 2014

Bunge Katiba.. UKAWA WAMJIBU KIKWETE!!

ukawa5 eeb08

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwataka wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) warudi bungeni akidai hawana sababu ya kwenda kushitaki kwa wananchi kwa sababu watawacheka na kuwasikitikia, umoja huo umemjibu wakisema wapo tayari kuchekwa.
Akihutubia vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) juzi, siku moja kabla ya sherehe za miaka 50 ya muungano, Rais Kikwete alisema kuwa huko nje wanakotaka kwenda UKAWA siko na siku yake sio sasa, hivyo akawaomba wasipoteze fursa hiyo muhimu ya kutoa mawazo yao bungeni ili yafanyiwe kazi.
Alisema wananchi hawahusiki wala hawana namna ya kuwasaidia kwani mengi ya hayo yanayowakasirisha ni matatizo waliyoyazusha wao.
Mwenyekiti wa UKAWA, Freeman Mbowe, aliliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa
kama Kikwete anafikiri kwamba watarudi bungeni kwenye mijadala ya dharau, ubaguzi na matusi inayofanywa na wajumbe wa CCM, basi hajui chimbuko la tatizo.
"Kadiri anavyoendelea kuliacha Bunge liendelee na mijadala ya kibaguzi na matusi, taifa linazidi kupasuka na washauri wake hawamwelezi tatizo hilo," alisema.
Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini atalitumbukiza taifa kwenye machafuko ingawa yeye anafanya utani kwa kuipasua nchi na kushangilia kauli za kibaguzi, kejeli na matusi zinazotolewa na baadhi ya wajumbe wa CCM.
"Rais na wasaidizi wake inaelekea hawajasikiliza hata kauli zinazotolewa na viongozi wa dini kuhusu rasimu ya Warioba, atuache twende kwa wananchi, wao ndio wataamua. Tumevumilia kwa kiwango fulani, lakini itafika mahali uvumilivu utaisha, kwani hatuwezi kuendelea kuzuiliwa kufanya mikutano na jeshi la polisi wakati mikutano ya CCM inafanyika kote nchini kutuchafua," alisema Mbowe.
Source: >>TANZANIA DAIMA<<

Sunday, April 13, 2014

BREAKING NEWS: MLIPUKO UNAOSADIKIWA KUWA WA BOMU WAITIKISA ARUSHA!!



Kitu kinachosadikika kuwa ni bomu kimelipuka Hapa Arusha maeneo ya MTK Bar Mianzini na kusababisha mshindo mkubwa sana.

Taarifa zinasema baadhi ya watu wameumia vibaya na wamekimbizwa hospitali za Mount Meru na Selian. Kwa sasa Jeshi la polisi limelizunguka eneo hilo kwa uchunguzi zaidi.. Bado hakuna taarifa ya vifo vyovyote vilivyotokana na tukio hilo. Taarifa zaidi tutaendelea kuwajuza..

BREAKING NEWS: Makamu wa Rais (Dk. Bilal), Kamanda Suleiman Kova, Mkuu wa Mkoa wa Dar na Dk. Magufuli wapata ajali ya helikopta!!

Katika kukagua uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua kubwa katika Jiji la Dar es salaam, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, Dk.John Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dar, Meck Sadiki na Afande Kova wamenusurika ajali ya helikopita iliyotokea leo Jijini Dsm.. 

Makamu wa Rais Dk Gharibu Bilal, Kamanda wa Kanda maalumu ya Dar Es Salaam, Sulemani Kova na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli wamenusurika katika ajali hiyo, na wamekimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi
Click image for larger version. 

Name: 7a485f354cb07268f3d727d1d35073da.jpg 
Views: 0 
Size: 73.5 KB 
ID: 151057
Click image for larger version. 

Name: 16c84ae9b714c405f2f16523a247c4f0.jpg 
Views: 0 
Size: 77.4 KB 
ID: 151058
Click image for larger version. 

Name: 3d4c4b635025850f151d4afc4c207bf7.jpg 
Views: 0 
Size: 32.6 KB 
ID: 151060





YALIYOMO KATIKA MAGAZETI YA LEO.. Jumapili, 13 April

Saturday, April 12, 2014

Mjue msanii wa Bongo aliyepata shavu kushiriki kwenye wimbo maalum wa Kombe la Dunia Brazil..!!

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Judith  Wambura ‘Lady JayDee’ kupitia kampuni ya Coca-Cola Tanzania  amepata nafasi ya kushiriki kwenye wimbo maalum kwa ajili ya michuano ya kombe la Dunia itakayofanyika Brazil  mwezi juni mwaka huu.



Katika hiyo ngoma Lady Jay Dee na David Correy wameimba kwa kutumia lugha ya kiingereza huku Octoppizo akiwa amerap kwa lugha ya kiswahili. Wimbo huo ambao umetambulishwa na Kampuni ya Coca Cola wakiwa wanazindua promosheni yao ya Kombe la Dunia itakayowezesha wateja wao kujishindia zawadi mbalimbali.

Cheki Video hii, Hillary Clinton arushiwa kiatu wakati akihutubia huko Las Vegas Marekani..

Wakati mke wa rais wa 42 wa Marekani, Bill Clinton akitoa risala huko Las Vegas Marekani kuna Mwanamke mmoja ambae hakujulikana ni nani, alitoka kwenye upande wa wanaosikiliza na kumrushia Hillary kiatu ambacho hata hivyo alifanikiwa kukikwepa.
Screen Shot 2014-04-12 at 5.13.27 AM
Imefahamika kwamba Mwanamke huyo hakua kwenye orodha ya waalikwa katika risala hiyo na walinzi walimshtukia kabla ya hicho kitendo ila kabla hawaja mdaka tayari alikua amesharusha kiatu.
Baada ya Hillary Clinton kufanikiwa kukiwepa aliweka utani kidogo watu wakacheka kisha akaendelea na risala wakati huo Mwanamke huyo ameshajisalimisha na kunyoosha mikono juu akiwa anatolewa nje ya ukumbi.
Video ya tukio lenyewe ipo hapa...

HAYA NDIO MATOKEO YA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA DAR....!