Blogger Widgets

Monday, September 16, 2013

Dr Mwakyembe Apangua Wajumbe wa Bodi ya Bandari (TPA)

Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe amepangua Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanznia (TPA) kwa kusitisha uteuzi wa wajumbe watano wa bodi hiyo. Imeelezwa kuwa wajumbe hao wameondolewa katika nafasi zao ili kuondoa migongano isiyo na tija ndani ya TPA.

Kwa mujibu wa taarifa waliondolewa ni Julius Mamiro, John Ulanga, Caroline Kavishe, Dk Hilderbrand Shayo na Asha Nassoro. Mbali na hao waliondolewa, mjumbe mmoja Dk Jabiri Bakari amejiondoa mwenyewe baada ya ombi lake la kufanya hivo, kukubaliwa Dk Mwakyembe. Waziri amewabakiza wajumbe wawili wa Bodi hiyo ambao ni Said Sauko na Jaffer Machano

Wajumbe wapya ni Mkuu wa mkoa wa Mtwara Joseph Simbakalia, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) Kipallo Kisamfu na mwakilishi wa wafanyakazi wa TPA ambaye hakutjwa jina. 

Source; gazeti la Habari Leo​