Blogger Widgets

Wednesday, October 23, 2013

SHULE ZA SEKONDARI NCHINI KUUNGANISHWA NA MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO..!!

0002_1ab10.jpg
Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa, akikata utepe wakati wa Uzinduzi wa mpango wa kuziunganisha shule za Sekondari na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ukianzia Shule ya Kambangwa Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Meneja wa Samsung Tanzania Kishor Kumar, wapili ni Mkuu wa kitengo cha mfuko wa huduma za jamii cha Vodacom, Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule,kutoka kushoto ni Mkuu wa shule hiyo Bi.Theresia Ng'wigulu.
0003_8d170.jpg
Waziri wa mawasiliano Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akimfuatilia mwanafunzi Frank Massay wa shule ya sekondari ya Kambangwa akitumia komputa zilizounganishwa na Mkongo wa taifa wa mawasiliano kwa ushirikiano wa Vodacom na Samsung. Pamoja nao katika picha (Kulia) ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za Jamii cha Vodacom Tanzania, Yessaya Mwakifulefule, Mkuu wa shule hiyo Bi.Theresia Ng'wigulu, na Mtaalamu wa komputa wa Samsung, Julius Giabe.
0004_05253.jpg
Waziri wa mawasiliano Sayansi na Teknolojia Profesa Makame, akimsikiliza kwa umakini Mkuu wa kitengo cha Huduma za Jamii cha Vodacom Tanzania, Yessaya Mwakifulefule wakati wa uzinduzi wa mpango wa kuunganisha shule za sekondari nchini na Mkongo wa taifa wa mawasiliano, uliofanyika kwa kuanzia na shule ya Msingi Kambangwa ya jijini Dar es Salaam.
0005_d4b71.jpg
Waziri wa mawasiliano Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akimfuatilia mwanafunzi Frank Massay wa shule ya sekondari ya Kambangwa akitumia komputa zilizounganishwa na Mkongo wa taifa wa mawasiliano kwa ushirikiano wa Vodacom na Samsung. Pamoja nao katika picha (Kulia) ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za Jamii cha Vodacom Tanzania, Yessaya Mwakifulefule, na Mtaalamu wa komputa wa Samsung, Julius Giabe.
0006_217d7.jpg
Wanafunzi wa shule ya Sekondari Kambangwa, wakitoa burudani kwa wageni waalikwa, Wakati wa uzinduzi wa mpango wa kuunganisha shule za sekondari na Mkongo na Taifa wa Mawasiliano.(P.T)