Blogger Widgets

Wednesday, May 14, 2014

UMESIKIA HII?? DIAMOND PLATNUMZ AZIDI KULA SHAVU,, Sasa amekuwa nominated kwenye tuzo za BET..!!



Baada ya msanii mkubwa wa Bongo fleva, Diamond Platnumz kuweka headlines mitaani kwa kushiriki kwenye tuzo za MTV base (Mama Awards), Amepata tena dili hili kubwa zaidi kuwahi kutokea kwa wasanii wa bongo. Sasa Diamond Platnumz ametajwa kuchaguliwa kushiriki kwenye tuzo za kituo kikubwa cha television cha marekani maarufu kama BET (Black Entertainment Television) ambapo yupo katika kipengele cha wanaogombea tuzo ya BEST INTERNATIONAL ACT AFRICA. Wasanii wengine katika kipengele hicho ni pamoja na Davido wa Nigeria, Mafikizolo, kundi toka Afrika kusini, Tiwa Savage wa Nigeria, Toofan na Sarkodie wa Ghana..

Katika kusibitisha hilo, BET kupitia page yao ya twitter walisibitisha kwa kumpongeza diamond kwa ujumbe mfupi..
BET DIAMOND PLATNUMZ 2014

Aljerry'12 inampongeza Diamond kwa dili kubwa hiyo.. Now go make Tanzania Proud...!!!!