Blogger Widgets

Monday, September 1, 2014

IKIWA LEO NDIO MWISHO WA USAJILI ULAYA,, HUYU NDIO NYOTA ALIYESAJILIWA NA MAN UTD LEO..!!!

IMG_6909.PNG
Leo ndio siku ya mwisho ya usajili barani ulaya na kila klabu ipo katika harakati za kuimarisha timu zao.
Klabu ya Manchester United leo hii imezishinda Manchester City, Real Madrid, Arsenal katika mbio za kusaka saini ya mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia Radamel Falcao.
United ambayo juzi ilikamilisha usajili wa Angel Di maria, leo imekamilisha usajili wa Falcao kwa mkataba wa mkopo wa mwaka 1 ambao una gharama ya £12m.
Falcao anategemea kutua jijini Manchester leo jioni kwa ajili ya vipimo vya afya na kusaini mkataba.