Sunday, June 14, 2015
NA HII NDIYO LIST YA WASHINDI WOTE WA TUZO ZA KTMA..
Bendi Bora ya Mwaka - FM Academia
Wimbo bora wa kushirikiana/kushirikishwa - MwanaFA ft. Ali Kiba - Kiboko Yangu
Msanii Bora Chipukizi Anayechipukia - Barakah Da Prince
Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Tanzania - Waite - Mrisho Mpoto
Wimbo bora wa Zouk/Rhumba - Ntampata Wapi - Diamond Platnumz
Wimbo bora wa Afro-Pop - Mwana - Ali Kiba
Video ya bora ya muziki ya Mwaka - Mdogo Mdogo - Diamond Platnumz
Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka bendi - Amoroso
Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka Bongo Flava - Nahreel
Mtunzi bora wa mwaka Hip Hop - JohMakini
Mtunzi bora wa mwaka bendi - Jose Mara
Mtunzi bora wa mwaka Bongo Flava - Ali Kiba
Mtunzi Bora wa mwaka Taarab - Mzee Yusuf
Wimbo Bora wa Afrika Mashariki - Sura Yako - SautiSol
Msanii Bora wa Hip Hop - JohMakini
Rapper bora wa mwaka bendi - Ferguson
Wimbo bora wa reggae/dancehall - Maua Sama
Wimbo bora wa Hip Hop - Kipi Sijasikia - Prof Jay ft. Diamond Platnumz
Wimbo Bora wa R&B - Sisikii - Jux
Wimbo Bora wa Kiswahili Bendi - Wale Wale - FM Academia
Wimbo Bora wa Mwaka - Mwana - Ali Kiba
Wimbo bora wa Taarab - Mapenzi Hayana Dhamana - Isha Mashauzi
Muimbaji Bora wa Kiume Bendi - Jose Mara
Mwimbaji Bora wa kike Taarab - Isha Mashauzi
Mwimbaji Bora wa Kiume Taarab - Mzee Yusuf
Muimbaji Bora wa Kike Bongo Flava - Vanessa Mdee
Muimbaji Bora wa Kiume Bongo Flava - Ali Kiba
Mtumbuizaji bora wa muziki wa mwaka wa kike - Vanessa Mdee
Mtumbuizaji bora wa muziki wa mwaka wa kiume - Ali Kiba
Monday, June 8, 2015
UMESIKIA HII YA WAGOMBEA WA CCM KUKIMBIA MDAHALO?? SIKIA HAPA..!

Leo June 08 2015 kulikuwa na mdahalo wa Wagombea wa Urais TZ ambao wanawakilisha CCM.. Mdahalo ulianza saa moja jioni Hyatt Regency Dar lakini Wagombea wengi hawakufika aliyefika ni Mgombea mmoja tu, Balozi Amina Salum Ali, wapo waliotoa sababu za kutofika lakini wengine hakukuwa na taarifa yoyote.
Ali Mufuruki ni mwenyekiti wa Waandaaji wa Mdahalo huo, hiki ndio alichokisema baada ya kutokea kwa hali hiyo. ”Tumesikitika kwamba wamejitoa.. Hiki ni kitu ambacho kimetuchukua muda mrefu sana kukiandaa. Sijui na sijapata nafasi kuzungumza nao nini kimewakuta“
“Tarehe 18 kutakuwa na mdahalo wa watu wa UKAWA… Hatuwezi kuwalazimisha kuja, wakiamua kutokuja hatuwezi kufanya chochote“
“Mzee Sumaye anauguliwa kwa hiyo hakuwepo hapa mjini… Mheshimiwa Nyalandu alithibitisha kushiriki leo asubuhi lakini ameenda Mbeya kikazi na leo usiku atasafiri kwenda nje ya nchi”
“Kinana alifafanua kuhusu hili jambo kwamba kila mtu ana hiari ya kuhudhuria ama kutokuhudhuria. Sidhani kama kuna tatizo kwenye chama… Sijapewa sababu ya hawa ambao hawajahudhuria”
Subscribe to:
Posts (Atom)